Advertisements

Thursday, December 8, 2016

DK MEDARD KALEMANI AFANYA ZIARA MIKOA YA RUVUMA, NJOMBE, IRINGA NA MOROGORO KUKAGUA MIRADI YA UMEME

 Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (katikati) akizungumza na wananchi wa Kata ya Ulaya wilayani Kilosa, Mkoa wa Morogoro, kuhusu utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini (REA II na REA III), wakati wa ziara yake wilayani humo hivi karibuni.
 Diwani wa Kata ya Ulaya wilayani Kilosa, Matokeo Kenedi (kushoto), akimweleza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (kulia) mahitaji ya umeme kwa wananchi wa Kata yake, wakati wa ziara ya Naibu Waziri kukagua miradi ya umeme wilayani humo hivi karibuni. Kulia kwa Naibu Waziri ni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Hassan Saidy.
 Nehemia Magendege kutoka Kijiji cha Ng’uruhe, Kata ya Pomerini wilayani Kilolo, akitoa maoni yake kuhusu utekelezwaji wa Miradi ya Umeme Vijijini (REA II na REA III) kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (hayupo pichani), wakati wa ziara yake wilayani humo hivi karibuni.
 Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza (kushoto), akiwasilisha taarifa ya Mkoa wake kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (kulia-mwenye miwani). Naibu Waziri na Ujumbe wake walifika Ofisini kwa Mkuu huyo wa Mkoa hivi karibuni, kabla ya kuanza ziara mkoani humo kukagua utekelezaji wa Miradi ya Umeme.
 Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Mugoyi Adam (wa pili kutoka kulia), akizungumza na wananchi wa Kata ya Ulaya (hawapo pichani), wakati wa ziara ya Naibu Waziri, Dk Medard Kalemani (kulia) wilayani humo hivi karibuni, kukagua miradi ya umeme.
Kaimu Mganga Mkuu wa Kituo cha Afya cha Kata ya Ulaya wilayani Kilosa, Dk Edmund Mjengwa (kushoto), akimueleza Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dk Medard Kalemani (kulia) mahitaji ya umeme katika Kituo hicho. Naibu Waziri ameelekeza Kituo hicho kiwe cha kwanza wilayani humo, kuunganishiwa umeme katika Mradi wa REA III.


No comments: