Advertisements

Saturday, May 27, 2017

JUMUIYA YA MADOLA YA WAPIGA MSASA WABUNGE KUTOKA NCHI 16.

Wajumbe wa Bunge la Umoja wa Bunge la Jumuiya ya Madola wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuaza kwa Mafunzo ya wiki moja yalioandaliwa na Bunge hilo, katika mafunzo hayo Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania limewakilishwa na Naibu Spika Dr. Tulia Ackson na Baraza la Wawakilishi Zanzibar limewakilishwa na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said.
Naibu Spika wa Jamhuri ya Muungano Dr Tulia Ackson pamoja na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Simai Mohammed Said wakishiriki katika masomo ya wiki pamoja huko Afrika Kusini University of Wits ambapo jumla ya Wabunge kutoka nchi 16 kutoka Jumuiya za Madola wameshiriki masomo hayo. 

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akiwasilisha kazi ya kikundi wakati wa mafunzo hayo ya wiki moja yanayofanyika Nchini Afrika Kusini yalioandaliwa na Umoja wa Bunge la Jumuiya ya Madola, akieleza kuhusiana na umuhimu wa kamati za kudumu za mabunge ya Jumuiya Madola kuelekea karne 21. 


Kutoka kushoto ni Mbunge kutoka India Ajay Misra, Naibu Spika Tanzania Dr Tulia Ackson, Seneta kutoka Jamaica Charles Pearnel na Mussa Dlamini Swaziland. Masomo hayo yanafanyika Johanessberg University of Witwatersrand kwa wiki moja na kudhaminiwa na Commonwealth Wealth. 
Wawakilishi kutoka Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Naibu Spika Dr.Tulia Ackson pamoja Simai Mohammed Said kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar wakiwa masomomi South Africa University of Witwatersrand wakibadilishana mawazo na Mbunge wa Swaziland Mhe Mussa Dlamini
Naibu wa Spika wa Jamhuri ya Muungano Dr Tulia Ackson akisikilizwa kwa umakini na washiriki wenzake. Kutoka kushoto Mhe.Simai Mohammed Said ( Zanzibar ) Pearnel Charles Junior ( Jamaica) Mussa Dlamini ( Swaziland ) na Ajay Misra ( India).
Waheshimiwa Wabunge wa Nchi za Jumuiya ya Madola wakiwa katika mafunzo  Nchini South Africa. wakifuatilia mafunzo hayo kwa makini. 
Wajumbe kutoka Mabunge ya nchi za Jumuiya ya Madola ( Commonwealth Countries) wakitembelea Mahakama ya Katiba ( Constitutional Court ) katika mji wa Johannesburg.
Mwakilishi wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar  Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa mafunzo hayo kutoka  kushoto  Mbunge wa Jamaica.Mhe.Heroy Clarke ( MP), Charles Pearnel Seneta pia akiwa Waziri wa Mambo ya ndani Jamaica, Stewart Michael ( MP) na Victor Wright ( MP ). 
Mjumbe kutoka Jumuiya ya Madola pia akiwa Mwakilishi kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said akibadilishana mawazo na Profesa David Everatt ambaye ni Kiongozi wa Skuli ya Utawala katika University of Wits, South Afrika. 
Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.Tulia Ackson akitoa nasaha zake za shukrani kwa niaba ya Wabunge kutoka nchi za Jumuiya ya Madola walioshiriki mafunzo hayo yaliofanyika katika ukumbi wa University of Witwaterstrand, Johannesburg South Africa.

No comments: