Advertisements

Sunday, May 28, 2017

NAHODHA WA TIMU YA SIMBA JONAS MKUDE APATA AJALI MOROGORO

NAHODHA wa Mabingwa wa kombe la Shirikisho na Kiungo wa timu hiyo, Jonas Mkude ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam. Anaandika Mroki Mroki-Mroki Mroki.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo ilipotokea ajali hiyo, Dumila katika shamba la Mitiki, zinaarifu kuwa hakuna watu wawili ambao bado majina yao hajapatikana wameumia na Mkude kupata majeraha madogo na kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi.


Watu hao walikuwa katika gari aina ya Toyota VX lenye namba za Usajili T 834BLZ na walikuwa wakitokea Dodoma kushuhudia fainali za kombne la Shirikisho la Soka Tanzania uliopigwa jana katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma uliozikutanisha Simba na Mbao.

Simba ilishinda mchezo huo kwa bao 2-1 na kutwaa ubingwa huo na kujipatoia tiketi ya kushiriki Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

No comments: