Advertisements

Friday, July 21, 2017

AMSHA AMSHA YA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZA SOKO LA EAC YASHIKA KASI

ROCK CITY MALL, MWANZA
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (The Foundation for Civil Society- FCS), Bw. Francis Kiwanga akitoa neno la ukaribisho kwa wageni waalikwa katika Kongamano la siku moja la kuwahamasisha vijana kuchangamkia fursa za Soko la Pamoja la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC). Kongamano hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa Rock City Mall jijini Mwanza tarehe 19 Julai 2017. 

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Mary  Onesmo Tesha ambaye alikuwa Mgeni Rasmi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. John Mongella akisoma hotuba ya ufunguzi kwenye kongmano la kuwhamasisha vijana kufanya biashara za kuvuka mipaka ya nchi za EAC. Mhe. Tesha aliwasihi vijana waondoe hofu na wajiunge katika vikundi ili waweza kufanya biashara kwa urahisi. Aliahidi kutoa milioni moja kwa kikundi kilichoundwa hapohapo kwa uratibu wa Mwkilishi wa Cloud Media, Bw. Samsonight Odera

Bi. Tesha akiendelea na hotuba yake.

Mchumi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw, Justin Kisoka akiwaeleza vijana wa Mwanza waliofurika kwenye ukumbi wa Rock City Mall sheria, kanuni na taratibu za kufuata kwa yeyote anayetaka kuanza biashara ya kuvuka mipaka ya nchi za EAC.

Mtaalamu wa Msauala ya EAC, Bw. Abel Maganya akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kuhusu kufanya biashara ndani ya Jumuiya ya EAC ikiwemo namna ya kupata cheti cha uasili na hati za kusafiria.

Mbinu mbalimbali zilitumika kufikisha ujumbe wa umuhimu wa kufanya biashara katika nchi za EAC. Hapa vijana wa Vipaji Foundation wakionesha kwa kutumia igizo baaadhi ya bidhaa zinazoweza kuuzwa katika nchi za EAC.

Mjasiriamali aliyefanikiwa ambaye pia ni maaruku wa kutoa mihadhara ya mbinu za kufanya biashara, Bw. James Mwang'amba akiwasilisha mada kuhusu mbinu za kuanza biashara na kuiendesha hadi ikakua kubwa.

Sehemu ya umati wa watu walioshiriki kongamano.

BABATI, MANYARA
 Msafara ulipokuwa unatokea Mwanza kwenda Arusha, ulisimama kwa muda Babati na kuongea na Wanababati namna ya kufanya biashara katika nchi za EAC.

Mkazi wa Babati akiuliza swali ili apate ufafanuzi kabla ya kuanza kupeleka bidhaa zake nchini Kenya

Vijana wa Vipaji Foundation wakitoa somo kwa Wanababati kupitia sanaa. 

Wanababati wakisikiliza kwa makini ujumbe wa namna ya kufanya biashara ya kuvuka mipaka.

No comments: