Advertisements

Monday, November 20, 2017

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA KATIBA NA SHERIA YATEMBELEA KIWANDA CHA SUKARI CHA MBIGIRI

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Stephen Kebwe akiwakaribisha baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria walipotembelea katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri kilichopo Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro Novemba 18, 2017.
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (watu wenye Ulemavu) Mhe. Stella Ikupa akisalimiana na Mhe. Siuleman Zedi mara baada ya kuwasili katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri kilichopo Wilaya ya Kilosa Morogoro.
Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe.Suleman Zedi akieleza jambo kwa wajumbe wa kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria (hawapo pichani) wakati wa ziara yao katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri mkoani Morogoro Novemba 18, 2017.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Stephen Kebwe akijibu hoja za wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria (hawapo pichani) walipotembelea katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri kilichopo Morogoro.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akifafanua jambo wakati wa mkutano wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria walipofanya ziara katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri Kinachoendelea kujengwa Morogoro.
Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe.Ally Sallehe (mb) akiulizwa swali wakati wa mkutano wa kamati hiyo ilipotembelea katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa katika gereza la Mbigiri Mkoani Morogoro Novemba, 18, 2017.
Mmoja wa wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Mhe. Taska Mbogo (mb) akichangia hoja wakati wa mkutano wa kamati hiyo walipotembelea katika Sukari na Kilimo cha Miwa katika gereza la Mbigiri mkoani Morogoro Novemba 18, 2017.
Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria wakifuatilia uwasilishaji wa mada kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe.Stephen Kembwe walipotembelea kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri Mkoani Morogoro Nobemba, 18, 2017.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Stephen Kebwe wakiangalia mashina ya miwa wakati wa ziara yaKamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri Wilayani Kilosa Morogoro.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na waandishi wa habari wakati wa ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri Morogoro.
Picha ya pamoja ya Baadhi ya Wajumbe wa Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria waliotembelea katika kiwanda cha Sukari na Kilimo cha Miwa Mbigiri Wilayani Kilosa Morogoro Novemba 18, 2017.

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

No comments: