Advertisements

Monday, November 20, 2017

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA OFISI YA MAKAMU WA RAIS


Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inakanusha taarifa inayosambaa katika Mitandao ya Kijamii kuhusu Taasisi ya Kiraia ijulikanayo kama Samia Habari Suluhu. Taasisi hiyo inajitambulisha kuwa inatoa mikopo ya fedha taslim, pikipiki na bajaji kwa wanawake wajasiriamali kwa masharti ya kuweka dhamana ya fedha taslimu shilingi laki mbili. Ofisi inapenda kuujulisha umma kuwa taarifa hizo ni za uongo na uzushi na zina lengo la kuupotosha umma wa Watanzania.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, hamiliki taasisi yoyote ya aina hiyo na hahusiki kwa namna yoyote na kazi za taasisi hiyo na wala haitambui taasisi hiyo.

Ofisi ya Makamu wa Rais inawataka Wananchi kuzipuuza taarifa hizo zinazosambaa kwenye mitandao ya kijamii kwani zinalenga kuleta taharuki na kupotosha Umma wa Watanzania.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Ikulu- Dar es Salaam

No comments: