Advertisements

Friday, January 19, 2018

Majina ya walioteuliwa na CHADEMA kugombea ubunge Kinondoni na Siha

Kamati Kuu ya Chama imemaliza Vikao vyake Leo tarehe 19 Januari, 2018 na imefanya uamuzi wa kushiriki kwenye uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Februari, 2018.
Baada ya uamuzi huu kufanyika , Kamati Kuu imewateua wagombea wa Majimbo hayo kama ifuatavyo;
1. Jimbo la Kinondoni ameteuliwa Mhe. Salum Mwalim Juma
2. Jimbo la Siha ameteuliwa Bwana Elvis Christopher Mosi
Wagombea wote wameshachukua fomu za uteuzi kutoka kwa wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo husika na watazirejesha kesho Jumamosi tarehe 20 Januari 2018 , kwa ajili ya uteuzi.

Imetolewa Leo tarehe 19 Januari, 2018.
John Mrema – Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje.

No comments: